Translate

Tuesday, July 31, 2012

DIAMOND HOI KITANDANI ASUMBULIWA NA KIFUA


Hii ni picha ya Diamond akiwa hospitali baada ya kubanwa ghafla na kifua na hivyo kwenda kufanyiwa uchunguzi ili kujua tatizo. Kwa mujibu wa Ommy Dimpoz ambaye ni mshikaji wake wa karibu tayari msanii huyo amesharuhusiwa lakini majibu ya vipimo vyake yatatoka kesho.

Miezi ya hivi karibuni Diamond amefululiza kufanya show katika mikoa mbalimbali bila kupata mapumziko ya kutosha na huenda hiyo ndio ikawa ni sababu.

Kupitia Twitter Diamond ameandika "Dah hali yangu si nzuri, naumwaaa."

Tunamwombea Diamond apone haraka.

No comments: