Translate

Friday, October 19, 2012

BAHADHI YA WAISLAM WAPAMBANA NA POLISI JIJINI DAR ES SALAAM LEO

Baada ya baadhi ya waumini wa dini ya Kiislamu kutawanywa kwa mabomu na askari wa Kikosi cha Kutuliza Ghasia hapo awali, kwa sasa waumini hao wanajipanga kuvamia kituo cha polisi mtaa wa Msimbazi wakiwa katika makundi makundi mikononi wakiwa na mawe na wakiimba nyimbo. Awali magari ya Jeshi la Wananchi yalipita mitaa ya Kariakoo yakiwa na wanajeshi waliokuwa wakiamuru wananchi kutawanyika lakini hali inaonekana kubadilika maana kwa sasa waumini hao wanajikusanya upya kutimiza azma yao ya kuandamana mara baada ya kumaliza swala ya saa 10 katika msikiti wa Idrissa uliopo Kariakoo. Baadhi ya madai ya waumini hao ni KUKAMATWA SHEIKH PONDA, KUTOONEKANA KWA SHEIKH FARIDI WA ZANZIBAR NA KUKOJELEWA QURAN.

No comments: