Translate

Tuesday, June 25, 2013

"NITAKUFA KABLA YA KUFIKISHA MIAKA 40"...AUNT EZEKIEL

WAKATI vifo vikizidi kuwatafuna wasanii, staa wa sinema za Kibongo, Aunt Ezekiel amefunguka na kudai kuwa hawezi kuishi miaka mingi na atakufa mapema kuliko watu wanavyodhani.


Aunt Ezekiel alifunguka hayo juzikati alipokuwa akipiga stori na mwandishi wetu jijini Dar ambapo alibainisha kuwa akijitazama mustakabali wa maisha yake basi anaona kabisa kuwa hawezi kufikisha hata miaka 40 kabla hajafa.

“Daah! Sijielewi kabisa yaani kwa jinsi ambavyo najiona, nikifikisha miaka 40 ni bahati aisee, dunia sasa imebadilika sana,” alisema Aunt.

No comments: